Tuesday, August 14, 2012

OMY DIMPOZ ATOA SABABU ZA KUONDOKA TOP BAND

Msanii wa kizazi kipya Ommy Dimpoz amefunguka sababu zilizomfanya atoke kwenye kundi la muziki wa kizazi kipya lilokuwa likiongozwa na Tid .Alisema Hayo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na mwandishi wa www.uptowntz.blogspot.com kuhusu kile kinachodaiwa kutoka kwenye kundi hilo bila ya kuwa na maelewano na muanzilishi wa kundi hiyo

Alisema kuwa ameamua kutoka kwa sababu aliona ni wakati wake kutangaza jina lake pamoja na kukua kimuziki “Nimekaa kwa Tid kwa miaka mitano bila ya mafanikio yoyote na hakuna mtu aliyekuwa anamjua Dimpozi na wala kumsikia “ alisema

Dimpozi anazidi kufunguka kuwa baada ya kutoka kwenye kundi hilo alipata mafanikio kwa haraka na ameweza kujitangaza kimuziki na kupata maendeleo kutokana na muziki anaoufanya .Anasema kuwa hana bifu na msanii yoyote na anamshukuru Tid kwa pale alipomfikisha

0 comments:

Post a Comment