This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Tuesday, July 31, 2012

NEW HIT: Izzo Biznes ft. Belle 9 - UTARUDISHWA

Monkeyflip - MODESELEKTOR feat. Nazizi & Abbas

Mwasiti ft Ally Nipishe - Mapito (Official Video)

Mtangazaji wa Ebony FM Iringa ampiga msanii wa Hip Hop

Kupitia ukurasa wa Facebook msanii wa hip hop wa mkoani Iringa Man Kichefu, leo ameandika, ‘jana nliitwa na eddo ebony.fm cha kushangaza alinivamia na kuanza kunipiga akidai nimemchafua! Poa mi sina noma ila nachoweza kusema its only the weak need to prove his strength through force! My mom hits more than anyone I ever met!” Kufuatia status hiyo tumempigia simu Man Kichefu ili atueleze sababu ya yeye kupigwa na mtangazaji huyo. “Kuna harakati fulani za muzki wa nyumbani hapa, unajue eeh, jamaa (Ebony Fm) wanatudiss sisi wasanii wa hapa. Kwahiyo kitu kilichokuja kufanyika kuna ngoma fulani sababu sisi kuna studio yetu tumefungua , tumejichanga tu mimi na mshikaji wangu tumefungua studio ,tumetengeza ngoma moja kwahiyo hiyo ngoma tuliyoitengeza inaitwa ‘Himaya ya Mkwawa’ inaelezea historia ya muziki wa Iringa na watu wa Iringa wale wanausuport muziki na wasio usupport. Baada ya ngoma hiyo niliiyoifanya sababu nimeiweka tu kwenye internet jamaa wakaichukua ile ngoma kitu kama wakaisikiliza hivi lakini mimi nikawa sijui. Nikawa napewa tu taarifa kuwa jamaa anakutafuta kaongea sana redioni. Mwisho wa siku juzi akanipigia simu mimi nikaipokea tu kwa roho safi, ‘vipi bro, fresh fresh’ akaniambia ebana na shida na wewe njoo ofisini. Nikamwambia poa mimi nikaenda tu kwa roho safi. Ndio hivyo yanii nimeenda ofisini jamaa akaniita akaanza kunitukana pale anadai nimemchafua, kanivamia akaanza kunipiga. Na baadhi ya wafanyakazi wengine yaani walikuja wakawa wananishika wananiambai ebana twende huku tukaongee. Pale ofisini kwao kuna sehemu moja nyuma ya ofisi kuna kibanda cha kupumzikia hivi, akaniita pale njoo tuongee. Nimefika hapo ndo akaanza kunishambulia sasa mimi nikaona hili eneo si zuri sababu ni nyuma ya ofisi, nikakimbia nikaja nyuma ya ofisi. Nimekuja mbele ya ofisi baadhi ya wafanyakazi wenzake wakaja wakanishika bana twende huku wakawa wananirudisha tena kule ambako jamaa alikuwa ananipiga yaani!
Kitu nilichokifanya mimi, nimefungua kesi polisi kwasababu ya ulinzi wangu wa mbele au kitu chochote kitakachoenda kule mbele lakini pia mimi sitaki nimfunge ama nimfanye lolote yaani.”

Breaking:Wasanii wapiga marufuku matumizi ya ringtone zao,

Umoja wa wanamuziki wa Bongo Flava, Rhumba, Dance, muziki wa Injili na aina zingine leo umetoa agizo kwa makampuni yanayouza miito ya simu nchini pamoja na makampuni ya simu kuiondoa miitio hiyo ndani ya siku saba kuanzia leo mpaka pale watakapokubaliana mikataba mipya. Katika barua hiyo iliyoandikwa kwenda kwa waandishi wa habari na iliyosainiwa na wasanii zaidi ya 150 nchini, wasanii hao wameyataka makampuni ya simu kuondoa matangazo ya ringtone hizo kwenye radio, magazeti, tv, website na kwenye ujumbe mfupi wa simu. Hatua hiyo imechukuliwa na wasanii hao baada ya kubaini kuwa makampuni ya simu yanawanyonya kwa kiasi kikubwa kwa kuwalipa chini ya asilimia 10 ya mauzo ya ringtone hizo huku yenyewe yakibaki na zaidi ya asilimia 80. Wiki iliyopita mbunge wa Kigoma Zitto Kabwe aliliibua suala hilo bungeni na kudai kuwa imeundwa kamati itakayoangalia upya utaratibu wa mauzo ya ringtone. Press Release ndio hii. YAH: KUFUTA MIKATABA NA KUSIMAMISHA KUUZA MUZIKI WA BONGO FLEVA,GOSPEL,DANSI NA TAARABU KWENYE MITANDAO YA SIMU. Husika na kichwa cha habari hapo juu, Kwa ujumla wetu sisi Wasanii toka Tanzania tunaofanya muziki wa Gospel, Rhumba , Taarabu pamoja na Bongo fleva tumeamua kutoa agzio kwenu la kusimamisha mauzo ya kazi zetu za muziki katika mtindo wa Ringtone na Callertunes katika mitandao ya simu ya Vodacom, Zantel,Tigo na Airtel na kufuta mkataba tuliosaini kati yetu sisi Wasanii na Kampuni yako mpaka hapo tutakapokaa sisi kama wasanii, nyinyi kama wasambazaji wa muziki wetu, pamoja na Mitandao ya simu ili kuzungumzia namna mpya ya sisi na nyinyi tutakavyofanya kazi. Sababu ya sisi Wasanii kusimamisha na kufuta mikataba kati yetu na wanaofanya biashara ya kuuza maudhui yetu ni pamoja kampuni husika kushindwa kuweka wazi taarifa za mauzo ya nyimbo pamoja na kutolipa katika muda husika kama ilivyoanishwa katika mikataba husika. Sababu ya pili ni mitandao ya simu kuchukua kiasi kikubwa cha fedha ambacho ni asilimia themanini ya mauzo yote ya maudhui yetu, jambo hili linatuumiza na limetufanya tuendelee kuishi kwa kutegemea aina moja ya pato toka kwenye shoo. Hivyo tumeziagiza kampuni zote zinazofanya kazi ya kuuza maudhui yetu kutoa maelekezo kwenye mtandao husika kuwaelekeza kusimamisha mauzo ya kazi zetu za sanaa ndani ya siku saba kuanzia leo tarehe 30/07/12 ikiwa pamoja na kusimamisha matangazo yote yanayotangaza mauzo ya kazi zetu kwa njia ya Television , Radio , blogs, website, Magazeti na Ujumbe Mfupi wa maneno mpaka hapo tutakapofikia muafaka. Jumla ya wasanii 153 wameshasaini barua hizo na wengine wanaendelea kusaini. Mwisho tunawashukuru kwa ushirikianao wenu, na tunaambatanisha sahihi zetu ili kuonyesha uthibitisho wa umoja wetu katika jambo hili. Asante.

Monday, July 30, 2012

MILIONEA WA TUSKER PROJECT FAME SEASON 5.HUYU HAPA

Kwa mara ya kwanza mshiriki toka Kenya nchi ambayo inaandaa mashindano hayo kuibuka kua wa kwanza hii ni ndoto ambayo imeotwa mdamrefu sana na wakenya walio wengi Jana imetimia na kukamilisha mashindano ya awamu ya tano ya Tusker Project fame Anaitwa RUTH MATETE.
Majoz ya furaha tulishuhudia yakimtoka jana katika fainali hizo.Uptowntz inatoa pongez kwa mshindi huyo wa season 5.

Ben Pol alijua ‘Baadaye’ ya Ommy Dimpoz itakuja kuwa hit

Mara nyingi wasanii hupata fursa ya kusikiliza nyimbo za wenzao zinapokuwa kwenye hatua ya kutayarishwa. Ben Pol aliusikia wimbo wa Ommy Dimpoz kabla hata ya kutoka na kumwambia kuwa utakuja kuwa tishio. ‘Unakumbuka niliwahi kukuambia kuhusu 'Baadae ,ona bro ,sasa nchi yote inaimba 'Baaadaeee eeeh'...hongeraaaa!!!,” ametweet Ben Pol kumwambia Ommy Dimpoz. “Nakumbuka broo thanxxx,” alijibu Ommy. Baadaye ni wimbo wa pili wa Ommy Dimpoz kufanya vizuri baada ya kuhit pia na wimbo wake wa kwanza, Nai Nai aliofanya na Ali Kiba. Katika hatua nyingine Ben Pol amekuwa msanii wa kwanza Tanzania kuzungumzia habari ya msanii maarufu wa Marekani Frank Ocean kujitangaza kuwa ni shoga. “Frank ocean anatuweka watu kwenye wakati mgumu ,ametoa album kali huku amejitangaza kuwa yeye ni gay ,kumuacha kumsikiliza nayo ni ishu,da!” amesema. Hata hivyo hitmaker huyo wa ‘Nikikupata’ na mshindi wa tuzo za Kili, anaamini kuwa scandal hiyo haimpunguzii uwezo wake katika muziki. “Haishushi ,ila bado wabongo sisi hatuwaelewi mashoga (mimi mbongo pia) ,ameni-dissapoint kidizain flani ,ila he's a gud singr/writer.” Album ya Frank Ocean, Channel Orange ilikamata nafasi ya pili kwenye chart ya Billboard 200 na nafasi ya kwanza kwenye Billboard R&B/Hip-Hop Albums chart, kwa kuuza kopi 131,000 katika wiki ya kwanza.

Picha: Jason Derulo akiperform nchini Rwanda

Juz mwanamuziki wa Marekani Jason Derulo alitumbuiza kwenye uwanja wa Amahoro nchini Rwanda kwenye fainali za shindano la Primus Guma Guma SuperStar. Hizi ni baadhi ya picha za show hiyo.

Saturday, July 28, 2012

SOPRANO ANUSURIKA KUFA

Mkali wa R&B Hapa nchini Francis Ndumbaro a.k.a Soprano jana 27/7/2012 majira ya saa 4:30 Asubuhi amepata ajali maeneo ya Airport Das es Salaam.msanii huyo ambae anafanya vizuri na ngoma yake ya Happy Day alikua katika Pikipiki ya aina ya Bajaji. Chanzo cha Ajali ni Roli la kampuni ya Azam inayomilikiwa na Bakharesa likiwa katika harakati za kuovertake Bajaji aliyopanda msanii Soprano ndipo gari hilo lilipoigonga Bajaji hiyo kwa pembeni.
Mwanamziki huyo wa kizazi kipya alikua akitokea Nyumbani kwake Kiwalani Kijiwe Samli akielekea Studio kwa Producer aliyetambulika kwa jina la AMBA iliyopo maeneo ya Njiapanda Segerea. Mbali na msanii huyo walihusika pia watu wengine wanne katika ajali hiyo nao ni,Director wa kampuni ya kutengeneza Video ya Emedia anaitwa SAMAJAMA,wengine ni JABIR,STIVE na FESTO ambae ndio alikua Dereva wa Pikipiki hiyo aina ya Bajaji. Wote watano walijeruhiwa na kukimbizwa katika Hospitali ya AMANA Iiyopo maeneo ya Ilala Dar es Salaam. Hata hivyo msanii huyo anendelea vizuri na tayari amaesharuhusiwa kurejea Nyumbani kwake toka Hospitalini hapo. Akichapa story na Uptowntz.blogspot.com Soprano pia alinifahamisha juu ya Ujio wake mpya baada ya Happy Day na kuwataka mashabiki wake kukaa mkao wa kula kwa ajili ya Track hiyo iliyosimamiwa na mkali STIVE WHITE yenye mahadhi ya zuku.Haitosh hapo nilipata nafac ya kusikiliza Demo ya Bidhaa hiyo.Honest Bidhaa ni kali.kupitia uptowntz.blogspot.com.utapata habar zaid juu ya ngoma hiyo.

Sunday, July 22, 2012

Juacali aiokoa ndege dhidi ya ajali

Alipokuwa kwenye ziara yake barani Ulaya, mgenge Juacali aligeuka kuwa shujaa mjini Amsterdam, Uholanzi kwa kuizua ndege isipige mzinga kabla haijapaa. Issue ilikuwa hivi: Juacali ndo kwanza alikuwa amepanda ndani ya ndege iliyokuwa inatoka Amsterdam kwenda London. Alikuwa amepata siti ya dirishani. Alipochek nje aligundua kuwa injini ya kushoto ilikuwa inatoa moshi mweusi. Jamaa akagundua kuwa kuna tatizo. Mara moja aliwataarifu wahudumu warembo wa ndege hiyo kuhusu tatizo hilo na baada ya muda mfupi kila mtu aliambia atoke nje ya ndege. Marubani walikuwa waipaishe ndege hiyo bila kugundua tatizo hilo ambalo kama isingekuwa Juacali leo hii yangekuwa yanasemwa mengine. Uongozi wa uwanja huo wa ndege uliilipia safari yake na wakampa tiketi kumi za bure za first class ambazo anaweza kuzitimia ndani ya miaka mitano.

Mtoto wa Usher afariki dunia

Hatimaye mtoto wa kufikia wa Usher, Kyle Glover amefariki dunia, wiki mbili baada ya kujeruhiwa katika ajali ya boti. Mtoto huyo wa mke wa zamani wa Usher, Tameka Foster amefariki jana asubuhi kwenye hospitali aliyokuwa amelazwa mjini Atlanta. Kyle aligongwa na boti kichwani wakati akicheza kwenye ziwa Lanier kiasi cha kufanya ubongo wake ufe. Kwa muda wote huyo mtoto huyo alikuwa amewekewa mashine maalumu ya kumsaidia kuishi. Kabla ya ajali hiyo Usher, ambaye jina lake halisi ni Usher Raymond, alikuwa kwenye vita kali na mke wake huyo wa zamani ya kugombania watoto. Salamu za rambirambi zimetolewa na mastaa mbalimbali kwenda kwa familia hiyo wakiwemo Justin Bieber, Toni Braxton Eric Benet na wengine.

Naeto C azawadiwa Porsche kama zawadi ya harusi

Weekend hii rapper wa Nigeria Naeto C amefunga ndoa na Nicole Chikwe. Harusi yake ilihudhuriwa na watu maarufu na wazito nchini Nigeria akiwemo rais wa zamani wa Nigeria, Olusegen Obasanjo ambapo mama yake Naeto, Kema Chikwe alikuwa waziri wake. Katika harusi hiyo wanandoa hao walizawadiwa gari mpya aina ya Porsche Cayenne yenye thamani ya Naira milioni 11 ambazo ni sawa na shilingi milioni 110.
Zawadi hiyo ilitolewa na mmiliki wa kampuni ya Auto Lounge, Larry Onuegbu. Awali kulikuwa na taarifa kuwa hiyo ilikuwa ni zawadi iliyotolewa na D’Banj ambaye ndiye aliyemkabidhi hata hivyo.

Saturday, July 21, 2012

NEW HIT SONG Addicted by hussein machozi

Hussein Rashid well known as Hussein Machozi Ame release video yake mpya ya wimbo alioutoa wiki chache zilizopita unaoitwa Addicted. Video imefanywa na kampuni ya Ogopa ya nchini Kenya ambako Machozi anaonekana kukubalika zaidi ya anavyokubalika hapa bongo. Well, It is simple but good video kwa kuangalia vitu kama location, story na wahusika waliomo kwenye video. Kama wewe ni true fan wa Hussein najua utakua unafuatilia kazi zake zote, kama unaweza kuvuta kumbukumbu ya video ya hit song yake ya "Kwa Ajili Yako" unaweza kugundua kuwa huyu video model ambaye ameonekana kwenye video hii mpya "Addicted" ndio yule alieonekana katika Kwa Ajili yako. Mwanzo ilikuwa kwa ajili yake, and now uko addicted kwake, Hussein is there something special with her that we don't know? She is pretty tho, she deserves it. Nice Video Hussein

SUPER JAY PHOTOS JUNE JULY

SUPER JAY AKIWA NA PROFESSOR JAY PAMOJA NA RICH MAVOCO NDANI YA STUDIO ZA 87.5 BOMBA FM ZANZIBAR.
KATIKA ENTERVIEW KALI AMBAYO YULISIMAMA MEZA MOJA NA WASANII KIBAO WALIOKUJA KUFANYA SHOW YA JUNE JULAY PICHANI HAPO NI PRESENTER WA SHOW YA THE HITS JABIR SUPER JAY AKIWA NA PROF.JAY PAMOJA NA RICH MAVOCO.
BAADHI YA WASANII WALIOPAMBA USIKU HUO WA JUNE JULIY.PICHANI NI WASANII SHAMAZEE,BERRY BLACK NA LIL GETO.
SWALAMAAAA!!!HII NI SLOGANY AMBAYO KWA MSIKILIZAJI WA 87.5 BOMBA FM ATAKUA ANAJUA NAMZUNGUMZIA D&J FLASH WA PEKEE AKIWA NA MTANGAZAJI WA KIPIND CHA THE HITS CHA 87.5 BOMBA FM PAMOJA NA BABA NDUGU HAVY WEIGHT MC PROF JAY.
HAVY WEIGHT DJ WA 87.5 BOMBA FM DUSKO DALLA CREAM DALLA HOMY AKIWA NA HAVY WEIGHT MC PROF JAY NDANI YA BOMBA FM.
MKURUGENZI MTENDAJI WA 87.5 BOMBA FM ZANZIBAR GURU RAMADHANI AKIWA NA PROF JAY NDANI YA STUDIO HIZO ZA BOMBA FM.
MKURUGENZI MTENDAJI WA 87.5 BOMBA FM ZANZIBAR GURU RAMADHANI AKIWA NA RICH MAVOCO NDANI YA STUDIO HIZO ZA BOMBA FM.
MKURUGENZI MTENDAJI WA 87.5 BOMBA FM ZANZIBAR GURU RAMADHANI AKIWA NA LIL GETO NDANI YA STUDIO HIZO ZA BOMBA FM.

Monday, July 16, 2012

TANGAZA NASI.

Kwa bei Rahisi sana tunatangaza Biashara yako na kuifanya kua ya kimataifa zaid kwani Dunia imekua kijiji sasa kua mjanja Jitangaze kupitia http://uptowntz.blogspot.com.Pia kupitia Bomba fm Radio.Kua wa kwanza upate Punguzo la Bei katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Wasiliana nasi kupitia saidjabir2001@yahoo.com.or +255713674322.Wahi mapema.

HUU NDIO UJIO MPYA WA MON G

MON-G akiwa na DULLAYO. Msanii wa kizazi kipya Ally Ramandhani ‘Mon G’ wiki hii anatarajia kutambulisha wimbo mpya wa ‘Binadamu’ .Akizungumza Dar es Salaam mwisho mwa wiki hii Mon G alisema wimbo huo utaanza kusikika kwenye vituo mbalimbali vya redio nchini mara baada ya kuutambulisha wiki hii Msanii huyo alitamba kwamba wimbo huo utakuwa kivutio kwa mashabiki wa kizazi kipya kutokana na maudhui aliyoyatumia ambayo yanaelimisha jamii. Alisema wimbo huo ambao ameutunga mwenyewe una maana kubwa kwa binadamu wote si wa kuwasikiliza kwani kila mtu ana mambo yake anayoyataka bila ya kumuiga mtu . Mon G, alisema wimbo huo ambao ameurekodi katika studio ya E Motion Record, pamoja na kwamba inazungumzia mapenzi lakini pia imetungwa kwa umahiri wa kumfanya mtu apende kusikiliza mara kwa mara “Lakini pia baada ya wiki kama mbili hivi ninatarajia kuingia kwenye harakati za kuitengeneza video yake sina mpango wa kuwa na albamu kwa kuwa hazilipi “ alisema Nyimbo nyingine za msanii huyo alizozitoa awali ni Mtoto wa Dar, Damu yangu, Uko wapi na sasa amekuja na Binadamu

Selles Mapunda (Steps Entertainment) afiwa na baba yake

Muongozaji mkuu wa filamu za kampuni ya Steps Entertainment Ltd, Selles Mapunda amefiwa na baba yake leo. Mzee Mapunda Mingi Sellestine amefariki akiwa na miaka 72. Kupitia Facebook Mapunda ameandika: News just getting to you Selles Mapunda's fb pals that I have lost my dady mr (Mr. Mapunda Mingi Sellestine 72). Mr Mapunda died yesterday around 1:39 pm after a brief illness. He was flown to Mikumi mission Hospital few days ago after being first admitted at Green Dispensary, Mikumi, Morogoro. Mr Mapunda was a good pillar to the Ace Tanzanian Movie Director working for steps Entertainment ltd while he was alive. He was also reported to be very useful in shaping the movie career of Selles Business Inc. with priceless advice and care he gives the Tanzanian movie Director when needed. May his soul rest in peace.( R.I.P. MR. Mapunda Mingi Sellestine 1940-2012) — pamoja na Nishid Dharsi na 45 wengine. Mapunda ameshaandika na kudirect zaidi ya filamu 17 zilizouza zaidi nchini ambazo ni pamoja na Jacky and Poyoyo 1,2,3,4 & 5, Another Wife, Full Moon, Miracle of Love, Slave of Love, Illegal Sisters, Desperate Romance, One day, The Chase, Same Girl, Crazy Tenant, Best loosers, The Return, Tears from Mombasa n.k.

New Music: Lloyd Banks ft. Fabolous – Bring It Back

Sunday, July 15, 2012

KIGOMA ALL STARS WAMESHATUA K.TOWN

Wasanii wale wa bongo fleva waliotokea Kigoma hivi sasa wapo jijini tayari kwa show yao ya tarehe 17/07/2012. Wasanii hao ni kama Linex, Abdu Kiba, Mwasiti, Recho, Banana Zoro, Diamond, Ommy Dimpoz, Queen Dlyn, Macomandor..etc..Show hiyo itakuwa free katika uwanja wa Lake Tanganyika... Kwa pamoja wasanii hao wameshakamilisha Bidhaa yao ambayo imepikwa na mtayarishaji maarufu hapa Tanzania Tuddy Thomas.Bidhaa hiyo ambayo itazinduliwa July 17 mwaka huu imepewa jina la kiasili(LEKE DUTIGITE)Maana yake Acha tujidai.Huu ni mfano mzuri sana na wakuigwa ktk upande wa sanaa ya Bongo.
Pichani: Linex, Peter Msechu & Abdu Kiba

Afande Sele azijibu shutuma za 20 Percent

Afande Sele azijibu shutuma za 20 Percent
Uswahiba kati ya wasanii wawili wa Bongo Flava nchini, Afande Sele na 20 Percent umeingia dosari baada ya kutupiana maneno kila mmoja kwa nyakati tofauti kwenye vyombo vya habari. Maneno hayo yalianza wiki iliyopita baada ya Afande Sele kuzungumza na Clouds FM na kudai kusikitishwa na kitendo cha swahiba wake 20 Percent cha kugoma kutumbuiza kwenye tuzo za muziki za Zanzibar wakati alikuwa amelipwa pesa zote. Kufuatia mgomo huo, waandaaji walimpeleka lock-up msanii huyo na kubaki na laptop yake mpaka pale atakapowarudishia waandaji hao shilingi milioni moja waliyompa kwaajili ya kuperform kwenye tuzo hizo. Hatimaye jana 20 Percent alizungumza na kituo hicho cha radio kuhusiana na tukio lenyewe na kusema kuwa Afande Sele amechanganyikiwa na anasumbuliwa na njaa ndio maana anamlaumu. Akiongea kwa jaziba, 20 Percent amesema Afande Sele ni kama ‘mtoto’ na alimshangaa kufahamu kuwa alifika Zanzibar saa sita usiku bila kuwa sehemu ya kulala kutokana na waandaaji hao kuwa wababaishaji. Jana (July 14) Afande Sele ametoa maelezo marefu kuhusiana na sakata hilo kupitia Facebook. Hivi ndivyo alivyoandika: “Salaam Ndugu zangu wote mashabiki na wadau wa muziki wetu!! Tamko langu kuhusiana na lugha zilizotolewa na Twenty Percent kuhusiana na show yetu ya Zanzibar Music Award. Tulialikwa kwenye ZANZIBAR MUSIC AWARD, na kabla ya kazi makubaliano yote ya kazi kwa mujibu wa mkataba yalifuatwa, makubaliano hayo yalihusisha sisi kujigharamia gharama zote za nauli na Malazi (accomodation). Tulifika Zanzibar salama, tulipokua Zanzibar twenty alitaka agharamiwe huduma zote ambazo ni nje ya mkataba wetu, nikamuomba na kumsihi sana ndugu yangu aheshimu mkataba, asitafute matatizo kwani tayari mpaka wakati huu tuna kesi na Halmashauri ya Manispaa ya Moro ambayo kimsingi sikuhusika (nilishatolea ufafanuzi siku za nyuma). Lakini yeye alipingana na mimi, akanibishia na kunisukuma Mbele ya wageni na wenyeji wetu, wakiwemo Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seiph Ali Idi, Waziri Seiph Khatibu. Walikuwepo waadishi wa habari wa siku Nyingi Akiwemo Abubakari Liongo (idhaa ya kiswahili radio Ujerumani), Mkurugenzi wa ZENJI FM ndugu Tua Saidi Tua. Mimi Selemani Abdallah Juma Msindi sihusiki kwa namna yoyote, na tabia zisizo za kuridhisha zinazoonyeshwa na Ndugu yangu Twenty Percent, ambae nimekua nae nyumbani kwangu hata kabla ya Tuzo zake Tano (Kili Music Award) ambazo kazi hizo zote hizo kaandikia nyumbani kwangu siwezi kuwa na tatizo nae ni ndugu yangu kiimani na kikazi, hata kazi yangu niliyofanya nae kabla siku za nyuma "MBELE YAKO NYUMA YANGU" .. Kuna mstari Nilisema " ..Kuandika Rhyme kwenda Gym kimtindo kuonyesha Ugumu, bado unatakiwa uwe na nidhamu ya kweli, sio ya kumzuga Mwalimu, utajihukumu". Nimekua nikisisitiza nidhamu kwa Ndugu zangu woote toka enzi za Ghetto Boyz, Watupori na Mabwasha'Kingdom, ambao wengine hawafanyi sanaa, ila nipo nao kwenye Familia yetu kubwa hapa Tanzania. Nimesikitishwa na kitendo hicho. Siku zote nimekua mwenye kuhitaji suluhu kwa namna ya Amani. Verry sorry kwa wote ambao mmefadhaika kwa hilo. Tuendelee kuwa pamoja na msisite kutoa ushauri wenu, maoni ili Game letu lisonge. MUNGU ATUBARIKI. Asanteni sana. Selemani Juma Abdallah Mutabhazi Msindi. a.k.a Afande Sele (King of Rhymes)

New Music: D'Banj - Oyato

Tuesday, July 3, 2012

New Music Video: Willow Smith ‘I Am Me’

Willow Smith amekuja tena lakini mara hii akionekana kuwa amekua zaidi na sura ya baba yake ikionekana mno kwenye sura yake. Kwenye “I Am Me” Willow anajaribu kuwaambia watu wanaokosoa kwa uvaaji wake kuwa yeye ndivyo alivyo. ‘Watu hawapendi ninavyovaa,’ anasikika akiimba.

New Music: Keyshia Cole ft. Lil Wayne "Enough of No Love

Keyshia Cole ameungana tena na timu ya YMCMB ambapo leo July 2, ameachia rasmi single yake ya kwanza kutoka kwenye albam yake mpya Woman To Woman aliyomshirikisha Lil Wayne. Isikilize hapo chini.

Monday, July 2, 2012

Hatimaye Anderson Cooper akubali kuwa ni ‘shoga’

Hatimaye mtangazaji maarufu wa TV Anderson Cooper amekubali kuwa yeye ni shoga. Cooper ametoa tamko hilo katika email aliyomtumia mwandishi Andrew Sullivan. Kwenye barua hiyo ameandika: "The fact is, I'm gay, always have been, always will be, and I couldn’t be any more happy, comfortable with myself, and proud." Kwa muda mrefu kulikuwepo na story za chini chini kuhusiana na suala hilo na kwa sasa ameuweka hadharani ukweli wote. Anderson Cooper ni mtangazaji wa CNN wa kipindi cha habari cha Anderson Cooper 360° na ni miongoni mwa watangazaji wanaolipwa fedha nyingi zaidi duniani

New Music Video: 50 Cent – I Aint Gonna Lie (Dirty)

Wakati leo ndio siku ambayo albam yake mpya ‘Murder By Numbers’ itatoka, usiku huu 50 Cent ameachia video ya wimbo wake mpya I aint gonna like. Itazame.

Tuzo za BET zimetolewa alfajiri ya leo


Tuzo za BET zimetolewa alfajiri ya leo mjini Los Angeles na walioibuka na ushindi zaidi ni pamoja na Nicki Minaj, Kanye West, na of course, Mr and Mrs Sean Carter (Jay-Z na  Beyoncé).

Kwa picha za HD leo ulimwengu wa muziki umeshuhudia kutano rasmi mbele ya public la Kim Kardashian na Beyonce waliokuwa wameongozana na mabwana zao Kanye na Jay-Z.


Good Music ikiongozwa na Kanye aliangusha show ya nguvu kwa kuperform wimbo unaohit kwa sasa Mercy akiwa na Big Sean na 2 Chainz.

Performance nyingine imetoka kwa Usher, Nicki Minaj and 2 Chainz, Melanie Fiona, D’angelo(!), Rick Ross na wana Maybach Music Group, bila kumsahau Chris Brown.


Show hiyo pia ilitumika kumuenzi Whitney Houston ambapo wasanii kadhaa waliimba nyimbo zake akiwemo Monica, Brandy (walioimba “I’m Your Baby Tonight” na  “I Wanna Dance With Somebody”), mama yake Whitney,Cissy Houston (aliyeimba  “Bridge Over Troubled Water”), na Chaka Khan, aliyeimba “I’m Every Woman.”
Hi indo list nzima ya washindi wa tuzo hizo;
Best Group: The Throne (Kanye West & Jay-Z)
Best Actor: Kevin Hart
Best New Artist: Big Sean
Best Male R&B Artist: Chris Brown
Best Collaboration: Wale ft. Miguel
Best Gospel: Yolanda Adams
Best Female R&B Artist: Beyoncé
Best Female Hip-Hop Artist: Nicki Minaj
Lifetime Achievement Award: Maze featuring Frankie Beverly
Video Of The Year: “Otis,” The Throne (Kanye West & Jay-Z)
BET Humanitarian Award: Rev. Al Sharpton
Viewers’ Choice Award: Mindless Behavior
Video Director Of The Year: Beyoncé & Alan Ferguson
AOL Fandemonium Award: Chris Brown

TAMASHA LA ZIFF KUANZA RASMI JULAI 7-15

Mkurugenzi Mkuu wa Tamasha la Filamu za Majahazi Zanzibar (Zanzibar International Film Festival),Prof. Ikaweba Bunting (pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa kutangaza Ufunguzi rasmi wa Tamasha hilo ambalo linatarajiwa kuanza Julai 7 - 15 katika viwanja vya Ngome Kongwe Kisiwani Zanzibar.Tamasha hilo kwa Mwaka huu linatarajiwa kufunguliwa na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Mh. Dk. Ali Mohamed Shein huku Mgeni Maalum akitarajiwa kuwa Muongozaji wa Filamu kutoka Hollywood,Mario Van Peebles aliewahi kung'ara katika filam za American Most Wanted,New Jack City na nyingine nyingi.Wengine pichani ni Waratibu wa Tamasha hilo,kutoka kulia ni Muslim Nassor,Robert Monondoli na Sabrina Othman Faraji.

PIPI AWEKA HADHARANI UJAUZITO WAKE


Wakati watu maarufu Duniani wakilipwa fedha nyingi na majarida mbalimbali kutoka nchi za Magharibi,imekuwa Tofauti sana kwa hapa Nchini mara baada ya Mwanamuziki Pipi Kuonyesha Tumbo lake Hadharani.

Sunday, July 1, 2012

BEEF KWA UPANDE MWENGINE.

 
Wakiwa wamepewa dau la $1 milli kila mmoja ili wapande stage kuzichapa live, Chris Brown na Drake wameendelea kutupiana mbovu kiasi ambacho kinazidi kuchochea zaidi beef lao.
Inaonekana ugomvi huu usiishe soon baada ya Chris Brown kumdiss Drake kwenye ngoma ya The Game iitwayo I don’t Like.
Kuna sehemu anasema “Wanarusha chupa, narusha mamodel sababu nampa Malaya pipe ndefu. Ntakuwa naimba, atakuwa anaimba, kwahiyo ni pambano, lakini subiri, simwoneshi mchizi taa ya kijani.

 “A fuck ni**a, that’s that shit I don’t like/ They throwin’ bottles, I’m throwin’ models just ’cause I give a bitch long pipe,” raps Breezy. “I be singin’, he be singin’, so it’s on, fight/ But hold up, I ain’t give a ni**a no green light/ This head up, my bread up, one on one, what you scared, bruh?/ Matter fact, take care bruh, you a pu**y ni**a/ My ni**a Tunechi, yeah that ni**a nice/ Shout out to Nicki, man, that ass tight/ Them eyebrows, man, them shits is yikes/ OVO, you overdosed, screamin’ YOLO no, I live twice.

SIHITAJI MARAFIKI FID Q.

Fareed Kubanda aka Fid Q kesho ataachia video ya wimbo wake mpya uitwao ‘Sihitaji Marafiki’ aliomshirikisha mwanadada Yvonne.


Video hiyo imefanywa na kampuni ya Showbiz Defined iliyochini ya Mike T.

Huenda video hiyo inaweza kurudisha heshima ya kampuni ya Showbiz ambayo hivi karibuni ilikuwa kwenye vita kali kutokana na Mike T kutupiana maneno na director wake wa zamani, Eryne Epidu.

Ugomvi huo ulipelekea Epidu arudi kwao Uganda na kudai kuwa Mike T alimchomea kwa uhamiaji.

Naye Ngosha The Don mwishoni mwa mwezi uliopita alitangaza kuwa ile show yake ya online ya Fid Style Friday itaanza kuoneshwa rasmi kwenye TV za Afrika Mashariki mwezi huu.

Hayo yatakuwa ni mafanikio makubwa kwa rapper huyo mkali nchini kwakuwa show yake itaweza kuangaliwa na watu wengi zaidi.