This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, June 21, 2012

BBA: Prezzo aomba arudishwe kwenye eviction




Hiki kiburi cha Prezzo ni kiboko! Eti kisa hataki kumshukuru Goldie kwa kumwokoa kwenye nomination ya kutolewa, sasa anamtaka Biggie kama vipi amrudishe tu ili waafrika waamue kama watambakiza ama watamchinjia baharini.

WASTARA ATOA HABARI MPYA ZA SAJUKI


Maombi ya watanzania pamoja na michango yao ya fedha vimesaidia kumfikisha mwigizaji Sajuki hapa alipo baada ya kupata nafuu kubwa toka apelekwe India kuitibiwa.
Wastara akizungumza exclusive na Jabir Super Jay kupitia ngomazetu.blogspot.com amesema Sajuki anaweza kuanza kuigiza hata sasa kwa sababu nguvu imesharudi, anaweza kutembea kwa muda mrefu na hata hali yake ya sasa imebadilika sana tofauti na mwanzo.
Amesema “baada ya miezi mitatu Sajuki anaweza kuanza kuigiza kama yeye mwenyewe atapenda na hata sasa hivi alipo pale unaweza kwenda nae location hana wasiwasi wowote ila kwa sababu ni mtu amefanyiwa upasuaji anahitaji kupumzika zaidi huwezi kutoka nae kwa sababu kuigiza inahitaji akili zaidi lakini baada ya miezi mitatu au minne anaweza kuendelea na kazi zake kama kawaida”
kwenye sentensi nyingine Wastara amesema hawezi kuzuia Sajuki kupigwa picha za Tv na magazeti kwa sababu kupitia vyombo hivyo vya habari ndio walifahamu kwamba anaumwa na wakaamua kumchangia sasa ni lazima wajue pia anaendeleaje kupitia vyombo hivyo hivyo.

Beyonce amwandikia barua shabiki wake kipofu

Beyonce amwandikia barua shabiki wake kipofu



Beyonce amemwandikia barua ya wazi shabiki wake Timmy Kelly, aliyezaliwa na upofu wa macho.

Mwanamuziki huyo alikutana na Timmy kwa mara ya kwanza wakati kijana huyo akiwa na miaka 13, backstage kwenye tuzo za Grammy.

Timmy kidogo amlize Beyonce baadaya kumwimbia wimbo wake Irreplacable, na hamjamsahau hadi leo.


Baada ya kubaini kuwa Timmy ambaye kwa sasa ana miaka 18 amehitimu high school na amechaguliwa kujiunga na chuo, Bey ameandika barua ya kumpongeza kwa hatua hiyo.

“Mara ya kwanza nimekutana na Timmy ilikuwa mwaka 2007, backstage kwenye Grammys. Alikuwa na miaka 13 na aliugusa moyo wangu kwa sauti yake na mapenzi yake kwa muziki na maisha,” ameandika Beyonce.

“Sasa hivi ana miaka 18 na amehitimu high school – Najinua sasa kwake!”
"Timmy alizaliwa kipofu. Lakini hili halikumtatiza. Amethibitisha kwa kila mmoja kuwa kila kitu kinawezekana kama ukijiamini na kujituma.” 

"Mjini Philadelphia anajulikana sana kama bahati kwa Eagles na kila anapoimba wimbo wa taifa kwenye mchezo timu hiyo hushinda.”

"Uwezo wake na kujituma kwake unavutia. Timmy alikubaliwa kujiunga na chuo kikuu cha Boyer kusoma muziki na dance.”

Thursday, June 14, 2012

WEMA SEPETU SIJALALA NA MORACKA



 
Queen kutoka tasnia ya filamu Bongo, Wema Abraham Sepetu, ametupilia mbali madai ya ‘star’ wa muziki wa kizazi kipya nchini Mohamed Hassan, ‘Moracka’ kuwa amewahi kutoka nae kimapenzi.
Akizungumza ‘live’Wema aliyewahi kushikilia ‘crown’ ya umalkia wa Tanzania amefunguka kuwa, kamwe hajawahi kufikiria kufanya jambo hilo kwa Moracka ingawa alikiri kuwa mara kadhaa nyota huyo alikuwa akimsumbua akimuomba kudondoka nae ‘on bed’..

“Ni kitambo kidogo kabla sija shinda taji la miss Tanzania, nakumbuka alikuja kuniomba kufanya nae video ya wimbo wake nafikiri hayo ndiyo yalikuwa mazungumzo yetu ya mwanzo…

  kinyume na hapo tumekuwa tukizungumza kawaida na kamwe sijawahi kuthubutu kutoa nguo na kumpa mwili wangu Moracka alisema Wema.

Juzi kati kupitia kipindi kinachorushwa na TV maarufu hapa nchini Moracka alifunguka kuwa amewahi kutoka kimapenzi na wema Sepetu kitambo kabla mwanadada huyo hajanza kujiachia na watu wengine maarufu akiwemo nyota wa Bongo fleva Nassib Abdul Diamond.

Kanye West apost picha ya ‘utupu’ ya Kim Kardashian Twitter!!




Juzi usiku Kanye West aliwashangaza followers wake wa Twitter kwa kupost kwa bahati mbaya picha ya mwanamke ambaye kwa haraka ukimwangalia utamuona anafanana na mpenzi wake Kim Kardashian.
Picha hiyo inamuonesha mwanamke akiwa amekaa kwenye kiti, akiwa uchi na akionekana akila chakula huku akiipa mgongo kamera.

Wakati sura ya mwanamke huyo haionekani full, anaonekana kuwa kama ni mpenzi wake na Kanye, Kim.


Kwa mujibu wa mtandao wa MediaTakeOut, Kim alichukia kwa kitendo hicho cha Kanye kushare picha yake kwenye mtandao huo wa kijamii na kumuomba aitoe mara moja.

Kanye aliitoa picha hiyo japo story hiyo na Kim iligeuka kuwa mjadala mkubwa.

Kwa mujibu wa mtandao wa AceShowbiz, ilikuja kubainika kuwa picha hiyo ni ya nyota wa picha za ngono aitwaye Amia Miley, lakini amegoma kuthibitisha kama ni yeye.

"Apparently a naked photo of me eating is going viral.... as Kim Kardashian.... Im confused," aliandika kwenye Twitter.

Unadhani hiyo picha ni ya Kim kweli?

UPANDE WA PILI WA SHILINGI DOGO JANJA Vs MADEE

SHOW YA MILIONI MOJA MADEE ALINIPA CHINI YA LAKI MBILI.




Siku moja baada ya Dogo Janja kudaiwa kufukuzwa Tip Top Connection, ukweli halisi kuhusiana na uamuzi huo umewekwa wazi na yeye mwenyewe.
Sababu zilizotajwa na Tip Top Connection ni kwamba Dogo Janja alilewa sifa na kuwa mtoro shuleni.

Kwa mujibu wa interview (ya pili kufanyiwa baada ya kipindi cha Amplifaya cha jana) tuliyofanya naye kwa simu saa moja asubuhi leo (June 14) akiwa stand kurejea nyumbani,  uonevu na dhuluma ndivyo vilivyomchosha kuishi Dar es Salaam.

Anasema tangu aje Dar es Salaam hajawahi kusaidiwa chochote na Madee zaidi ya mambo ya muziki pekee huku kula, malazi na ada ya shule vikifanywa na rafiki yake Madee aitwaye Abdallah Doka ambaye (Dogo Janja) alikuwa akiishi kwake.

Anasema kutokana na ngoma zake kujipatia umaarufu alikuwa akipata show nyingi nchini na zote alikuwa halipwi chini ya milioni moja.
Kilichokuwa kinamsikitisha anasema ni kulipwa hela kidogo isiyozidi laki mbili na hivyo kumfanya aishi kwa tabu licha ya kuingiza hela nyingi za show.
“Nilikuwa navumilia tu bro kwasababu kila nilipolalamika kuhusu mambo ya hela Madee alikuwa mkali sana,” ameongea uchungu.

Dogo anasema ilikuwa inafikia wakati akifanya show za ukumbuni hulipwa elfu hamsini au chini ya hapo na wakati mwingine alikuwa halipwi kabisa.
Tamaa ilizidi kumwingia Madee kiasi cha kumnyang’anya kadi yake ya benki na kuanza kuchukua hela bila kujua password aliipata wapi.

“Kuna wakati nilikuwa nataka kumtumia mama laki moja, Madee akanikataza eti kwakuwa watadhani nina hela sana,” anasema.
Mpaka tunaongea naye asubuhi hii, anasema kadi yake imebakiwa na shilingi 25,000 tu.

Ameendelea kudai kuwa juzi Madee alimpigia simu na kumwambia kuwa kaka yake wa Kibaha ameandaa show ya CCM na atamlipa shilingi laki moja.
“Hivi kweli bro mimi ni mtu wa kufanya show ya laki moja?”. Hata hivyo aliamua kukubali ili kuepusha lawama.

Baada ya show kumalizika anasema yeye na back up artist wake walirudishwa saa saba usiku wakati asubuhi yake alitakiwa kwenda shuleni kuchukua namba ya mtihani na kuandaa dawati la kukalia.

Dogo Janja anaeleza kuwa inamuuma sana kwakuwa muziki haujampa chochote licha ya Madee ambaye huwa hapati hata show kumtumia kimaslahi na hadi leo hii anamalizia kujenga nyumba yake.

“Ni kama vile Madee alinipanda ili anivune.”

Ameendelea kusema kuwa hiyo juzi sasa hadi kufikia Tip Top watangaze kumfukuza alikuwa kwa Tundaman akipiga story na Madee akamuita kisha kuanza kumpiga.

Alichukua simu yake akaondoka nayo. “Jamaa alianza kujitumia meseji kutoka kwenye simu yangu kwenda kwake za matusi ama kuwa nataka kumroga. Jana nimemuonesha Milard hizo meseji na amesikitika sana.”

Anasema simu yake alipewa jana.

Kitendo cha kumwambia Madee kuwa amechoka na anataka kurudi nyumbani ndicho kimemfanya amfanyie yote hayo hadi kumwambia kuwa watahakikisha wanambania asifanye vizuri tena kwenye muziki. Pia amedai kuwa Madee aliwapigia simu wazazi wake ili wamkataze Dogo Janja asifanye interview na vyombo vya habari.

DOGO JANJA ARUDISHWA KWAO


Nyota wa muziki wa kizazi kipya  kutoka  ‘kruu’ ya  Tip Top Connection  yenye maskani yake pande za  Manzese  jijini  Dar  es  Salaam  Abdul Abubakar Chende  ‘Dogo  Janja’  ametupiwa  virago   ndani ya kundi hilo.
Akizumngumza na  Teentz .com mapema leo kiongozi wa kundi hilo Hamad Ally  ‘Madii’  amesema kuwa  Dogo Janja  ameshindwa  kuendana na  makubaliano halisi yaliyokuwepo baina yake na uongozi wa kundi hilo ikiwemo  kuhudhuria  shuleni kama alivyokuwa akitakiwa  kufanya kila siku  badala yake  amekuwa akiendekeza  starehe na  wakati mwingine kufanya mambo ambayo kwa namna moja ama nyingine yalikuwa yanalichafua kundi hilo.
“Tumemkabidhi kwa kaka yake mapema leo tukiwa  maeneo ya Ubungo tayari kwa safari ya  kurudi kwao  na wakati huo tulifanya mawasiliano na…
Nyota wa muziki wa kizazi kipya  kutoka  ‘kruu’ ya  Tip Top Connection  yenye maskani yake pande za  Manzese  jijini  Dar  es  Salaam  Abdul Abubakar Chende  ‘Dogo  Janja’  ametupiwa  virago   ndani ya kundi hilo.
Akizumngumza mapema leo kiongozi wa kundi hilo Hamad Ally  ‘Madii’  amesema kuwa  Dogo Janja  ameshindwa  kuendana na  makubaliano halisi yaliyokuwepo baina yake na uongozi wa kundi hilo ikiwemo  kuhudhuria  shuleni kama alivyokuwa akitakiwa  kufanya kila siku  badala yake  amekuwa akiendekeza  starehe na  wakati mwingine kufanya mambo ambayo kwa namna moja ama nyingine yalikuwa yanalichafua kundi hilo.
“Tumemkabidhi kwa kaka yake mapema leo tukiwa  maeneo ya Ubungo tayari kwa safari ya  kurudi kwao  na wakati huo tulifanya mawasiliano na baba yake  kumuarifu kuwa Tip Top   hatuko na mwanae kwa sasa”  alisema Madii
Katika hatua nyingine Madii  amesema kuwa Dogo Janja alilewa sifa na  kujisahau kufanya yale anayotakiwa kufanya ndani nanje ya kundi  kufuatia mafanikio ya muziki aliyoyapata akiwa  na Tip Top Connection kwani hivi karibuni alitega shule na kwenda kujificha  nyumbani kwa TundaMan  hukua akimuaga Madii kuwa anakwenda shule.
Kuona hivyo TundaMan aliamaua kumuarifu Madii na mara moja  kiongozi huyo wa kundi aliamua kwenda  kumsaka,  lakini baada ya dogo Janja kugundua kuwa Madii anakuja aliamua kukimbia na kwenda kujificha  uchochoroni lakini akiwa huko mafichoni bahati mabaya  alikanyaga  kuku  na  siri yake kujulikana kuwa amejificha hapao ndipo alipokamatwa na kuamriwa kufungasha kilicho chake  tayari kurejea ‘kileji’.
"vimekuwa ni vitendo vya kila mara kukacha kuhudhuria shule, tumechoka na hatukuwa na njia nyingine ya kufanya alisema Madii'

Monday, June 11, 2012

MAJUX Video